Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida
(Hospitali ya Mkoa)

HOSPITALI YA RUFAA MKOA WA SINGIDA YATOA MAFUNZO YA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZWA KWA WATUMISHI WAKE WOTE

Posted on: December 4th, 2021

Mafunzo hayo ya magonjwa yasiyoambukizwa yametolewa kwa muda wa siku 5 kuanzia tarehe 30/11/2021 hadi tarehe

04/11/2021 ambapo takribani watumishi 320 wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida Wamefanikiwa kupata mafunzo

hayo.

Wakiongea baada ya mafunzo hayo watumishi walioshiriki mafunzo hayo wamesema, wamefurahi sana mafunzo hayo

kutolewa kwa watumishi wote kwani mbali na kupata mafunzo juu ya udhibiti wa magonjwa yasiyoambukizwa washiriki

walisema wamepata fursa ya kujifunza namna ya kukabiliana na Ukimwi mahala pa kazi, namna ya kujikinga na ugonjwa

wa Corona, umuhimu wa kupata chanjo ya korona, umuhimu wa kutowanyanyapaa wagonjwa wa Ukimwi. Pia washiriki

walisema wamejifunza juu ya Haki na Wajibu wa Mtumishi wa Umma. Washiriki wa mafunzo haya wamesema elimu

waliyoipata watahakisha wanaitoa kwa watumishi wenzao hususani watumishi wa ajira mpya watakaokuwa wanapangiwa

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida bila kuzisahau familia zao.